Mwili wa mwanamke mmoja mwenye umri wa miaka 45 ulipatikana katika nyumba yake jumamosi kwenye kijiji cha Kaaga kaunti ya Murang’a. Mwanamke huyu anaaminika kuuawa na majambazi ambao baada ya kutekeleza kitendo hicho cha uhaini walitoroka na baadaye kumpigia simu jirani yake kumfahamisha kuhusu walichokitenda.