Safari ya ulezi kwa mara nyingi huwa imekabidhiwa kina mama, lakini kwa wanaume kutoka Tanzania , wao wameipuuzilia mbali dhana hii kwa kuuonyesha ulimwengu mzima na haswa kenya kuwa ulezi sio wa kina mama pekee. Na kupitia miradi ya mashirika kamavile amref, mwanamume amefunzwa jinsi ya kujitolea ili kupunguza idadi ya wanawake wanaofariki kutokana na matatizo ya uzazi. Mwanahabari Saida Swaleh alizuru taifa la Tanzania na kutuandalia sehemu ya kwanza ya kibirikizi cha uzazi Tanzania.