Vyama vya walimu nchini vya Knut na Kuppet vimetishia kuitisha mgomo wa waalimu au kufungwa kwa shule za umma kufuatia hali ya sintofahamu inayokumba sekta ya elimu baada wizara ya fedha kushindwa kutoa fedha zinazofadhili elimu ya bure katika shule za msingi na shule za upili . Ukosefu wa fedha hizo zinazokisiwa kufika takriban shilingi bilioni tisa imepelekea kuzorota kwa masomo katika shule hizo.