Chama cha walimu nchini KNUT kimetoa ilani ya mwezi mmoja kwa serikali kutimiza ahadi yake ya kutoa nyongeza ya marupurupu ya 200% la sivyo walimu watagoma ifikapo tarehe 1/7/2012. Katibu mkuu wa KNUT David Okuta amesema ni sharti serikali kuwakumbuka waalimu katika makadirio ya kifedha ya mwaka 2012/2013 ili kutimiza mkataba huo walioafikiana mnamo mwaka wa 1997.