Mapema leo viongozi na wasomi kutoka maeneo ya Pokot wametoa makataa ya siku saba kwa kamishna wa polisi Mathew Iteere kueleza kuwachukulia hatua maafisa wa GSU, walionaswa katika ukanda wa video wakimtendea unyama mkubwa, kijana mmoja wa kipokot. Ktn leo imebaini kuwa kijana huyo kwa jina Joseph Loling'areng anaishi katika kijiji cha Chekata, huko Kwanza, na bado anauguza majeraha. Joseph alitendewa unyama huo, mwaka 2009, katika kambi ya GSU ya kerita.