Watch KTN Live http://www.ktnkenya.tv Siasa ni mchezo wa nipe nikupe. Msemo unaowiana na yale mabadiliko ya baraza la mawaziri jana. Kulingana na wachambuzi, Rais Kibaki alitilia maanani suala la ICC, alipobadilisha mawaziri wa mrengo wa Pnu. Alitaka wandani wake ndio washikilie wizara muhimu zenye uhusiano na suala la ICC, ili wafuate mkondo anaoutaka. Kwa Raila Odinga- kumtimua Najib Balala, kunachambuliwa kama kuendeleza ile siasa yake ya usipofuata nyayo, utakiona cha mtema kuni. Kabla ya wino wa wachambuzi kukauka, dhana ikatiliwa pondo, na kuteuliwa kwa Ali Hassan Joho kama naibu waziri wa uchukuzi. Kwa ufupi wachambuzi wanasema Rais Kibaki na waziri mkuu waliangalia maslahi yao, walipofanya mageuzi hayo