Waziri wa Elimu Profesa Sam Ongeri alikabiliwa na wakati mgumu bungeni, kuhusiana na kufutiliwa mbali jkwa matokeo ya wanafunzi 1000 kutoka mkoa wa Kaskazini Mashariki. Ongeri alikuwa anatoa taarifa ya wizara alipowaelezea wabunge kuwa kulikuwa na ushahidi wa kutosha kuwa watahiniwa hao walifanya udanganyifu katika mtihani huo wa ksce mwaka uliopita, na ndio sababu matokeo yao yalifutiliwa mbali.