Serikali ya Tanzania huenda ikaondoa ada inayoyatoza magari ya kubeba mizigo kutoka humu nchini yanayoingia nchini humo. Hatua hii inalenga kuondoa kizuizi cha kusafiri kwa watu katika kanda ya afrika mashariki kwa mataifa yaliyo wanachama wa jumuiya ya afrika mashariki. Tangazo hili litaiendeleza kanda ya afrika mashariki kibiashara. Akitoa tangazo hili katika mpaka wa kenya na tanzania hapo namanga, waziri wa jumuiya ya afrika mashariki wa tanzania samuel sitta amesema ada hiyo ilikuwa ikitatiza shughuli za kibiashara na eneo la kusini humu barani afrika. Kenya na tanzania zinafanya mikakati ya kubuni kamati katika mpaka wa namanga itakayoshughulikia shughuli za kibiashara. Punde tu kamati hiyo itakapobuniwa biashar