Wenyeji wa Lamu hii leo wameandamana kupinga mpango wa ujenzi wa bandari mjini humo wakidai mradi huo utasababisha baadhi yao kufurushwa kutoka katika mashamba yao. Bandari hiyo mpya inalenga kupunguza mrundiko katika bandari ya mombasa. Hata hivyo katibu wa usafiri cyrus njiru alipuuzilia mbali uwezekano wa watu kufurushwa akisema kwamba wachache watakaoathirika watalipwa fidia. Mbali na hayo kuna habari njema kwa wale ambao mizigo yao imezuiliwa bandarini mombasa kwa kushindwa kulipiwa kwani sasa, malipo yameondolewa kati ya sasa na tarehe tatu mwezi ujao.